Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson amekutana na kufanya
mazungumzo na Rais wa Urusi, Vladimir Putin leo Jijini St. Petersburg nchini
Urusi ambapo wamejadili kuhusu namna bora ya kuimarisha amani duniani.
Akizungumzia kuhusu mgogoro unaoendelea baina ya Urusi na
Ukraine, Dkt. Tulia amesema kabla ya kuzungumza na Rais Putin, tayari
walishazungumza na maspika wa nchi hizo mbili, ambapo wao kama IPU wamezungumza
naye kama kiongozi wa nchi katika sura ya kuiziweka nchi hizo mbili pamoja.
Pamoja na mambo mengine, Dkt. Tulia amesema wao kama Umoja wa Mabunge Duniani, wanatarajia kutengeneza fursa ya mabunge ya Urusi na Ukraine kuweza kuzungumzia amani katika maeneo yao ya utawala.
0 Maoni