Ujumbe wa wataalam wa UNESCO, wakutana na Wahadzabe, Wadatoga na Wairaqw

  

Wataalam wa shirika la UNESCO waliowasili Tanzania kuhalalisha tena Jiopaki ya Dunia ya UNESCO Ngorongoro-Lengai, wametembelea tarafa za Karatu na Eyasi na kukutana na jamii ya Wairaqw, Wahadzabe na Wadatoga katika kuangalia utekelezaji vigezo vya UNESCO katika kulinda tamaduni za kipekee, jiolojia na ikolojia ya urithi wa eneo hilo.

Katika ziara yao hiyo iliyoanza jumatatu ujumbe huo ulitembelea eneo la Makumbusho ya UNESCO Jiopaki ya Ngorongoro-Lengai na kutembelea shule ya awali na ya msingi ya lugha ya Kingereza ya Tumaini na kisha shule ya awali na ya msingi ya lugha ya Kingereza Father Lieberman zote zilizopo Karatu kuangalia jitihada za utoaji elimu zenye kuwajengea msingi vijana kuwa walinzi wa jiopaki.




Chapisha Maoni

0 Maoni