Msarifu wa Taasisi ya Benjamin William Mkapa, Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema
Taasisi ya Benjamin William Mkapa itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali
kwa kuchangia kuandaa nguvu kazi, kuwaendeleza na kuboresha mifumo kupitia
programu ya Mkapa Fellows katika sekta ya afya.
Dkt. Mwinyi aliyasema
hayo leo tarehe 31 Julai 2024 wakati wa kumbukizi ya tatu ya Hayati Benjamin William
Mkapa katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini
Dar es Salaam.
Aidha Rais Dkt. Mwinyi ameleeza kuwa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar inatarajia kujenga Hospitali ya Rufaa ya Binguni itakayokuwa na
vitanda 600 hivi karibuni.
Halikadhalika Rais Dkt. Mwinyi amesema SMZ imetoa ajira mpya
1,050 za watumishi wa afya, imejenga
jumla ya nyumba 80, 16 kila wilaya zilizogharimu shilingi bilioni
20 ili kuboresha mazingira ya kazi kwa
watumishi wa sekta ya afya na kuwapa motisha ya kazi.
Vilevile Rais Dkt. Mwinyi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwa juhudi anazochukua za kuboresha sekta ya afya nchini.
0 Maoni