Rais William Ruto wa Kenya amevunja baraza la mawaziri
pamoja na kumuengua Mwanasheria Mkuu Justin Muturi, kufuatia shinikizo la maandamano ya vijana kuipinga serikali.
Katika uamuzi wake huo alioutangaza hivi punde, ni waziri
mkuu aliyesalimika, Musalia Mudavadi, ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya
Nje wa Kenya.
Rais Ruto amesema atawahusisha wadau wengine wa vyama vya siasa katika mchakato wa kuunda baraza la mawaziri.
Pamoja na mambo mengine Rais Ruto amesema kuanzia wizara zote zitakuwa chini ya Katibu Mkuu Kiongozi.
0 Maoni