Wananchi wa Kata ya Mtipwili na Chiwanda Wilayani Nyasa
wamekumbwa na taharuki baada ya Kiboko Kuvamia mashamba na kula mazao ya
mihogo, mpunga na viazi katika Vijiji vya Chiulu, Kwambe, Mtipwili na Malini.
Wananchi hao wametoa kero inayowakabili, katika Mikutano ya
Hadhara katika Vijiji hivyo ambapo Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mh. Peres Magiri
anafanya Ziara ya Kikazi ya Kukagua Miradi ya maendeleo, Kusikiliza na kutatua
kero za wananchi, kupitia Kampeni yake “Kijiji kwa Kijiji”.
Wananchi hao wamefafanua kuwa, moja ya kero inayowakabili
ni uharibifu wa mazao ya chakula yanayoharibiwa na viboko ambao wapo wawili,
wanaotembea pembezoni mwa Ziwa Nyasa katika kata ya Mtipwili na Chiwanda hivyo
kuwapa wasiwasi mkubwa wa mazao na uhai.
Awali wametoa Taarifa Ofisi ya Maliasili na wataalam wamefika, zaidi ya mara mbili na kutofanikiwa kumuona.Hivyo Mh. Mkuu wa Wilaya tunaomba utusasaidie kutatua kero hii ili tuweze kuwa na amani.
Diwani Viti maalum Kata ya Chiwanda,Catherine Mawila amethibitisha mbele ya Mkutano huo, ni kweli
kero hii inawasumbua sana wakazi wa wa Kata ya Chiwanda na Mtipwili na kuwataka
kutoa ushirikiano kwa Askari wa Mali Asili wanapofika mkatika maeneo yao.
“Ni kweli tatizo hili lipo na linawakabili wananchi wa Kata
hizi mbili za Mtipwili na Chiwanda, ila wakija askari huyu kiboko haonekani na
wakiondoka anaonekana sasa sisi wananchi tunatakiwa kutoa ushirikiano,” alisema
Diwani Mawila.
Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mh. Peres Magiri amesema anaichukua
kero hii na kwenda kuifanyia kazi ili kutatua changamoto hii, kwa haraka
iwezekanavyo ikiwa ni pamoja na kuwataka Askari wa Maliasili kuja kukaa kwa
muda mrefu ili waweze kuwaua Viboko.
Aidha, amewaagiza wananchi kufanya kazi kwa juhudi kwa
kutotegemea mazao ya uvuvi pekee bali wajikite kwenye kilimo cha mahindi, maharage,
soya, mbaoga mboga, na mazao mengine yanayostawi katika mazingira hayo.
Na. Netho sichali- Afisa Habari wilaya ya Nyasa
0 Maoni