Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Doto Biteko
amesema mikoa ya Katavi na Kigoma iko mbioni kuunganishwa katika Gridi ya Taifa
kutokea mkoa wa Tabora tarehe 07 Julai 2024.
Ameyasema hayo wakati akikagua maendeleo ya njia ya
kusafirisha umeme ya msonngo wa kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Katavi na Kituo
cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Ipole Mkoani Tabora.
Aidha, ametoa rai kwa wananchi kuilinda miundombinu ya umeme.
0 Maoni