Mfanyabiashara maarufu Tanzania Bilionea Yusuf Manji ambaye
aliwahi kuwa Mwenyekiti na Mfadhili wa Klabu ya Yanga, anatarajiwa kuzikwa leo
huko Florida nchini Marekani.
Manji alifariki dunia jumamosi usiku katika hospitali ya
Florida, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na mtoto wake Mehbub Manji.
Mehbub amewashukuru watu mbalimbali wakiwamo Watanzania ambao wameendelea kuomboleza kifo cha baba yao, na kuwashukuru kwa maombi yao.
0 Maoni