Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua ameonesha dalili ya
kuwa mambo si shwari baina yake na Rais William Ruto.
Hata hivyo, Gachagua amesema masuala yanayowakwamisha katika
uhusiano wake na Rais Ruto, yanazungumzika katika moyo wa kuimairisha
maendeleo, umoja na demokrasia.
Amesema mgawanyiko serikali ya Kenya Kwanza, unachochewa na
watu waliojiunga na serikali hivi karibuni, ambao ndio wanaamua namna wale
waliokuwa na Rais Ruto katika nyakati nzuri na mbaya wanawezea kushirikiana na
rais.
Kwa mujibu wa gazeti la Nation la Kenya, kama hiyo haitoshi katika kuonyesha mgawanyiko Gachagua atafanya mdahalo wake pekee na kundi la vijana wa Gen Z, kuhusu masuala ya utawala wa serikali, nje na ule ulioandaliwa na Rais Ruto.
0 Maoni