Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na
Muungano wa Tanzania maendeleo mengi yamepatikana katika sekta tofauti zikiwemo
za kijamii, kiuchumi, kisiasa na kidiplomasia.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipofungua Kongamano la
kumbukumbu ya Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano wa Tanzania
lililoandaliwa na Chuo cha Utumishi wa Umma Zanzibar (IPA) kwa kushirikiana na
Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt.Salim Ahmed Salim (CFR) kutoka Dar es
Salaam katika ukumbi wa Dkt.Mohamed Ali Shein Kampasi ya Tunguu, Mkoa wa Kusini
Unguja tarehe: 11 Juni 2024.
Aidha Rais Dk. Mwinyi ametoa rai kwa washiriki wa kongamano
hilo kuzungumzia sera zinazopewa kipaumbele katika mipango mikuu ya Serikali
zikiwemo za Uchumi wa Buluu, Uwekezaji, Diplomasia ya Uchumi na kutoa
mapendekezo yao kwa Serikali.
Kwa upande mwingine Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kujenga jengo la Chuo cha Utumishi wa Umma Zanzibar (IPA).
0 Maoni