Baadhi ya wafanyabiashara wa eneo la Kariakoo Jijini Dar es
Salaam wamefungua maduka yao huku baadhi yao wakiendelea kufunga, kushinikiza
kutatuliwa kero zao zilizopelekea kuitishwa kwa mgomo.
Hali hiyo imechangiwa na kauli ya Mwenyekiti wa
Wafanyabiashara Kariakoo, Martin Mbwana ya kuwaachia uamuzi wa kufunga au
kufungua maduka katika eneo hilo mikononi mwa wafanyabiashara hao.
Wakati huo huo gari la matangazo limekuwa likipita leo mitaa tofauti ya Kariakoo kuhamasisha wafanyabiashara kufungua maduka yao, huku wakisisitiza kuwa kero mbalimbali zao zinaendelea kufanyiwa kazi.
0 Maoni