Wachezaji wa sarakasi nyota Ramadhani Brothers wamefikisha tuzo
za America’s Got Talent katika hifadhi bora barani Afrika Serengeti baada ya
kuzifikisha katika kilele cha Afrika, kilele cha Uhuru (Mita 5985) hifadhi ya
Taifa Kilimanjaro.
Vijana hawa wanaendelea kutangaza utalii wa Tanzania ikiwa ni juhudi moja wapo za kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutangaza utalii wa duniani.
Washindi hao wa za America’s Got Talent, hivi karibuni pia walifanikiwa kukwea hadi kileleni mwa Mlima Kilimanjaro, wakiwa na tuzo hizo za @agt katika mwendelezo wa kuvitangaza vivutio vya utalii vya Tanzania.
TANAPA inakukumbusha kuendelea kupigia kura Hifadhi ya Taifa
Serengeti na Mlima Kilimanjaro
𝗝𝗶𝗻𝘀𝗶 𝘆𝗮 𝗞𝘂𝗽𝗶𝗴𝗮 𝗞𝘂𝗿𝗮
Fungua tovuti ya
www.worldtravelawards.com/vote
0 Maoni