Hospitali ya Taifa Muhimbili imepokea msaada wa mashine
POCUS yenye thamani ya TZS. 16.9 MIL kutoka kwa wafadhili wa mradi wa Himofilia
(Novo Nordisk Foundation na Novo Nordisk Haemophilia Foundation) ambayo
itahudumia wagonjwa wenye magonjwa ya damu (HIMOFILIA).
Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji,
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba MNH, Dkt. John Rwegasha amesema mashine hiyo
itatumika katika kufanya uchunguzi na kufuatilia maendeleo ya ugonjwa katika
maungio ya wagonjwa na kusaidia kupunguza matumizi ya dawa yasiyokuwa ya lazima
kwa wagonjwa wa Himofilia kwakuwa sio kila maumivu aliyonayo mgonjwa
yanayosababisha na kuvuja damu.
Ameongeza kuwa mashine hiyo itawezesha mtalam kuona kama
mgonjwa amevuja damu sehemu za ndani mathalani kwenye goti, tumboni au misuli
kwa urahisi na haraka ambapo ingekuwa ngumu kutambua kwa macho.
Ameongeza kuwa pamoja na kutoa msaada wafadhili hao pia
wataendesha mafunzo ya siku nne ambapo yataanza tarehe 28 hadi 31 Mei, 2024
ambapo yatatolewa kwa wataalam wa Utengamao.
“Ninawashukuru Wafadhili wetu Novo Nordisk Foundation na Novo Nordisk Haemophilia Foundation kwa uwezeshaji wao kwani pamoja na kutupatia msaada pia wametuletea mtaalam aliyebobea zaidi katika mashine hiyo ya POCUS kutoka nchini Kenya ambaye atawejengea uwezo wataalam wetu namna nzuri ya kutumia mshine hiyo,” amesema Dkt. Rwegasha.
0 Maoni