Mama Mariam Mwinyi atoa mkono wa Eid kwa wazee na watoto yatima

 

Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mhe.Mama Mariam Mwinyi ametoa wito kwa Waumini wa Dini ya Kiislamu  kuendelea  kutenda mema , kuombeana baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na  kuendelea kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu.

Mama Mariam Mwinyi amesema hayo alipotoa zawadi za mkono wa Eid alipotembelea vituo mbalimbali vya kuwalea Wazee na Watoto ikiwemo kituo cha kulea Watoto  ZASO Fuoni Mambosasa,  kituo cha Wazee Welezo , kituo cha Wazee Sebleni , kituo cha  Watoto SOS na kituo cha  Watoto Mazizini , Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe: 10 Aprili 2024.

Aidha, Mama Mariam Mwinyi amesema ni wajibu kuwalea, kuwatembelea na kuwaenzi Wazee kufanya hivyo ni baraka kubwa sana.

Halikadhalika Mama Mariam Mwinyi ameeleza kuwa Serikali itaendelea kuwasaidia Wazee na kuwajali.


Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mhe.Mama Mariam Mwinyi akitoa mkono wa Eid kwa watoto yatima.

Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mhe.Mama Mariam Mwinyi akifurahia jambo pamoja na mtoto aliyembeba.

Chapisha Maoni

0 Maoni