Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dk Emmanuel
Nchimbi , amewataka Watanzania wote kujituma na kufanya kazi kwa bidii huku kutojihusisha na vitendo vya kutoa au
kupokea rushwa.
"Endeleeni kuchapa kazi kwa bidii , kufanya kazi
zitakazokuingiza kipato kihalali lakini jiepusheni na rushwa kwakuwa siku zote
ndio adui wa haki, kuchapa kazi ni kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais Samia
za kuwataka Watanzania wote kufanya kazi na ndipo tutazidi kulijenga taifa letu
na kuimarika kiuchumi"
Vilvile, Balozi Balozi Nchimbi amesema Jeshi la CCM (Viogozi
wa kitaifa) wataendelea kuhakikisha wanaisimamia serikali ipasavyo katika
kutimiza wajibu wao na kutekeleza ilnai ya uchaguzi ya mwaka 2020/2025.
Balozi Nchimbi ameyasema hayo wakati alipopokelewa na vongozi, wanachama, wapenzi, mashabiki na wadau mbalimbali wa maendeleo katika ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya.
0 Maoni