Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipewa maelezo na Mratibu wa
Shughuli za Vijana mkoa wa Dodoma Almas Daruwesh kuhusu majukumu mbalimbali
yanayoratibiwa na Chama cha Skaut, wakati wa Mkutano wa wadau wa elimu mkoa wa
Dodoma kwenye ukumbi wa Chuo cha Biblia Mkoani Dodoma Machi 25, 2024. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akioneshwa na Mwalimu Selina Kadewele wa Shule ya Msingi Songambele-Kongwa zana ya kufundishia (Mfano wa Komputa mpakato) wanafunzi wa awali wakati wa Mkutano wa wadau wa elimu mkoa wa Dodoma katika ukumbi wa Chuo cha Biblia Mkoani Dodoma Machi 25, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akioneshwa na Mwanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya wasichana ya Msalato, Rosemary Brighton namna wanavyofanya mafunzo kwa vitendo ya upasuaji, wakati wa Mkutano wa wadau wa elimu mkoa wa Dodoma kwenye ukumbi wa Chuo cha Biblia Mkoani Dodoma Machi 25, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipokea tuzo, kutoka kwa watoto
Shule ya Msingi Kizota, kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia Suhulu Hassan, ikiwa
ni kumshukuru kwa jitihada anazofanya katika miundombinu ya elimu, kuimarisha
taaluma na michezo, kwenye mkutano wa wadau wa Elimu uliofanyika katika ukumbi
wa Chuo cha Biblia Mkoani Dodoma Machi 25, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipokea tuzo, kutoka kwa Dada Mkuu wa Msalato Girls, Sylvia Florence, inayotambua juhudi zake katika usimamizi na utekelezaji wa miradi ya elimu nchini, kwenye mkutano wa wadau wa Elimu uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Biblia Mkoani Dodoma Machi 25, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
0 Maoni