Watakaopandisha bei ya sukari Nyamagana kukiona

 

Serikali wilayani Nyamagana Jijini Mwanza imewaonya wafanyabiashara wa sukari watakaojaribu kukiuka bei elekezi kutoka bodi ya sukari iliyotolewa kwenye tangazo la serikali inayoelekeza mfuko wa kilo hamsini wa bidhaa hiyo uuzwe laki moja na elfu arobaini huku kilo moja ikiuzwa kwa shilingi elfu mbili mia nane hadi elfu tatu

Agizo hili limetolewa leo tarehe 8/3/2024 na Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Aidha, Makilagi amewataka pia watendaji wa serikali kusimamia kikamilifu bei ya bidhaa hiyo ili wananchi waipate kikamilifu.



Chapisha Maoni

0 Maoni