Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.
Dk. Hussein Ali Mwinyi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa bega kwa bega tangu Mzee Mwinyi alipoanza
kuugua mwezi Novemba alipopelekwa Uingereza kwa matibabu.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo jana katika hitma na Dua Maalum
ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi ilyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika viwanja vya maonesho Nyamanzi, Mkoa wa
Mjini Magharibi, Unguja.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi amewashukuru pia Madaktari wa
Hospitali ya Mzena kwa kazi kubwa waliyoifanya kujaribu kuokoa maisha ya Mzee
Mwinyi pamoja na Masheikh, Waalimu, Ndugu, Marafiki na wananchi kwa dua nyingi
walizomuombea Mzee Mwinyi kwa kupindi chote alichokuwa akiugua na baada ya
kufariki.
0 Maoni