Rais Dk. Mwinyi amshukuru Rais Dk. Samia

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa bega kwa bega tangu Mzee Mwinyi alipoanza kuugua mwezi Novemba alipopelekwa Uingereza kwa matibabu.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo jana katika hitma na Dua Maalum ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi ilyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika viwanja vya maonesho Nyamanzi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi amewashukuru pia Madaktari wa Hospitali ya Mzena kwa kazi kubwa waliyoifanya kujaribu kuokoa maisha ya Mzee Mwinyi pamoja na Masheikh, Waalimu, Ndugu, Marafiki na wananchi kwa dua nyingi walizomuombea Mzee Mwinyi kwa kupindi chote alichokuwa akiugua na baada ya kufariki.



Chapisha Maoni

0 Maoni