Kamati ya Bunge yaridhia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu 2024/2025

 

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imeridhia Mpango na Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu na taasisi zilizopo chini ya ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2024/25.

Aidha, Kikao cha kamati hiyo kilichofanyika jana bungeni jijini Dodoma kikiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Fatuma Toufiq ambapo ameipongeza Wizara hiyo kwa kuandaa bajeti ambayo itawezesha utekelezaji wa majukumu sambamba na kuleta mageuzi katika sekta ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.

Katika kikao hicho Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako ameongozana na Naibu Waziri wa ofisi yake Mhe. Patrobas Katambi pamoja na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Mhe. Mhandisi Cyprian Luhemeja kuiongoza Menejimenti na Wakuu wa taasisi zilizopo chini ya ofisi hiyo kuwasilisha bajeti hiyo.



Chapisha Maoni

0 Maoni