Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Ombeni Manase Kilawa
(43) mkazi wa Lusese Wilaya ya Mbarali kwa tuhuma za kumuua mke wake aitwaye Happynes
Gervas Mwinuka (40) mkazi waKijiji cha Lusese kwa kumkata na kitu chenye nchakali.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Machi 13, 2024
Kitongoji cha Masista, Kijiji cha Lusese, Wilaya ya Mbarali baada ya kutokea ugomvi
baina ya wanandoa hao wakiwa nyumbani kwao na kupelekea mtuhumiwa Ombeni Kilawa
kuchukua kisu na kumkata mke wake shingoni.
Akiongelea tukio hilo leo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga amesema
uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi baada
ya mtuhumiwa kumhisi na kumtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya mapenzi na wanaume
wengine.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, limetoa wito kwa jamii kuwa pindi
wanapopatwa natatizo au changamoto katika ndoa zao isiwesuluhisho lake
kujichukulia sheria mkononi bali ni kutafuta ushauri kwa wazazi, walezi,
wasimamizi wa ndoa, viongozi wa dini, katika madawati yajinsia na watoto waliopo
kila Wilaya ya Kipolisi, katika ofisi za halmashauri au kutafuta haki kwenye Mahakama
ili kuepuka madhara.
0 Maoni