Makamba awasilisha salamu za Rais Samia kwa Rais Kagame

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba, amewasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame katika Ikulu ya Rais, mjini Kigali.

Kupitia ujumbe wake aliouchapisha kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa  X, Mhe. Makamba ameandika.

“Niko katika siku ya mwisho ya ziara yenye tija kubwa nchini Rwanda, nikiambatana na ujumbe wa viongozi wakuu kutoka wizara mbalimbali. Rwanda ni jirani na rafiki yetu. Ziara yangu hapa ilithibitisha dhamira ya pamoja ya kuimarisha uhusiano wetu. Nimepata fursa ya kumtembelea Mheshimiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame na kuwasilisha salamu za bashasha kutoka kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” ameandika na kuendelea..Mwongozo wake juu ya kuendeleza uhusiano wetu ulikuwa wa busara.

Mhe. Makamba pia alikutana na Mawaziri wane akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje, ICT, Biashara na Kilimo - na timu zao.

“Tumeamua kuharakisha utekelezaji wa yale ambayo yalikubaliwa hapo awali na pia kuchunguza maeneo mapya,” ameandika Mhe. Makamba.

Amesema, zaidi ya asilimia 80 ya mizigo ya Rwanda inapitia bandari ya Dar es Salaam ikiwa na tani milioni 1.4 za mizigo na makontena 63,000 yaliyochakatwa bandarini mwaka jana.

Rwanda ni ya nchi ya 3 kwa watumiaji wengi wa bandari hiyo “Tumejitolea kuifanya bandari ya Dar es Salaam, iwe rahisi kwao kuendelea kuitumia kwa kufungua Ofisi za TPA mjini Kigali, pia tumetoa vipande vya ardhi kwa Rwanda kwa bandari kavu huko Isaka mkoani Shinyanga na Kwala mkoani Pwani.

Lakini pia Rwanda inatumia miundombinu ya BROADBAND ya Tanzania kwa kiasi fulani cha uwezo katika muunganisho wake.

Mhe. January Makamba ameendelea kuandika “Tumejitolea kuwa mshirika wa kutegemewa katika eneo hili na tunataka kupanua biashara hii. Tanzania ni mshirika wa pili wa kibiashara wa Rwanda.”

Amesema, uwezo wa kuwa wa kwanza upo. Tunakwenda kulifanyia kazi. Wanyarwanda wananunua nafaka nyingi kutoka Tanzania. Tumeamua kuhalalisha soko hili. Rwanda imewekeza katika kiwanda cha kuhifadhi kumbukumbu jijini Mwanza, ambapo wakulima watapata soko la faida la maziwa. Tumehakikisha mafanikio ya mradi huu

Chapisha Maoni

0 Maoni