Taasisi ya Utafiti wa
Wanyamapori Tanzania (TAWIRI)
imetangaza matokeo ya utafiti mbinu za
kudhibiti wimbi la popo Jijini Dar es Salaam ambapo imebainisha aina
tatu (3) za dawa kuonesha ufanisi sambamba na mbinu zisizo tumia dawa za
kuvalisha neti miti na kupunguza vichaka/matawi ya miti maeneo ya makazi.
Akizungumza na vyombo vya Habari Dkt. Julius Keyyu,
Mkurugenzi wa Utafiti TAWIRI amesema Taasisi hiyo imefanya utafiti kwa awamu
mbili ambapo utafiti wa awali ulijikita
kujua ukubwa wa tatizo, na utafiti wa awamu ya pili ulijikita kufanya majaribio
ya kuwadhibiti popo katika Jiji la Dar es Salaam.
Dkt. Keyyu ameeleza katika kuwadhibiti Popo, majaribio yamefanyika kuanzia mwezi Mei, 2023 katika Kata ya Kivukoni Jijini Dar es Salaam
ambapo njia za aina mbili zilitumika ikiwemo njia ya matumizi ya dawa na njia
zisizo za matumizi dawa.
Dkt.Keyyu amesema katika njia za matumizi ya dawa, aina tatu
za dawa zimeonesha ufanisi ambapo dawa
ya _Repells-All®_ ilionesha uwezo wa kuwadhibiti popo kwa siku zisizopungua 46
hadi miezi mitatu kutokana na hali ya hewa, dawa _Bat (CRP)_ ilionesha
kuwadhibiti popo kwa muda wa siku 12 hadi 31 na dawa ya _Industrial
Naphthalene_ ilionesha kudhibiti popo kwa siku 23.
Pia, Dkt. Keyyu ameeleza mbinu mbili zisizotumia dawa ambazo
zimeonesha kufanya vizuri ni njia ya
kuishungushia miti neti ambayo imeonesha ufanisi kwa asilimia 100% hasa
katika kuwadhibiti popo kuharibu miti ya
matunda na njia ya mbinu ya kupunguza miti matawi/ vichaka inaweza kudhibiti
popo kwa asilimia 30% hadi 50% kuendana na namna ya upunguzaji "kama
wanasayansi hatushauri njia ya
upunguzaji matawi au kukata miti kwakuwa si rafiki kwa mazingira"
amehimiza Dkt. Keyyu
Ikumbukwe, miongoni mwa madhara ya popo ni uchavuzi na uharibifu wa nyumba na vifaa, uharibifu wa mazao, usumbufu wa kelele na wakati mwingine hubeba vimelea vya magonjwa.
0 Maoni