Mapema leo asubuhi ndani ya ukumbi wa Bunge Spika wa Bunge
la Tanzania Mhe Dkt Tulia Ackson amentangaza Mh Esther Nicholas Matiko kuwa
mshindi wa jumla kwenye michezo ya Bunge Sport Bonanza 2024 lililofanyika Dodoma chini ya udhamini wa Bank ya Azania na
Qatar Airways kwa kumpatia Tiketi ya Ndege daraja la bishara (Business Class)
kwenda Nchi yoyote Duniani atakayoichagua kwa ajili ya Mapumziko kwa siku
atakazochagua yeye.
Mhe. Esther Nicholas Matiko ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu
kutokea Mkoa wa Mara ambaye na Shabiki wa Timu ya Simba ameibuka kidedea kwa
kujinyakulia Medali za Dhahabu Tatu (3) akiwakilisha Mashabiki wa Timu ya Simba
Sc kwa kuwashinda washindani wake ambao ni Mashabiki wa Timu ya Yanga.
Kumalizika kwa Bonanza hilo lililojumuhisha michezo
mbalimbali ikiwa ni michezo ya mtu mmoja mmoja na ile inayojumuhisha muunganiko
wa Timu, Mhe Esther Nicholas Matiko amekuwa Mchezaji pekee aliyejinyakulia
Medali nyingi zaidi ya wachezaji wengine zipatazo 7 (Medali 3 binafsi na Medali
4 za Timu) katika Bonanza hilo lililofanyika 27/01/2024 chino ya udhamini na
Bank ya Azania.
Mhe. Esther Nicholas Matiko ameibuka mshindi katika michezo
ya Karata Wanawake, Pull Table Wanawake, Mchezo wa Bao Wanawake na upande wa
Timu ameshinda Mpira wa Pete, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu na Riadha mita 100
Mhe. Esther Nicholas Matiko ameendelea kung’ara katika mashindano mbalimbali yanayojumuhisha Wabunge wa Tanzania na hata yale mashindano ya Mabunge Afrika ya Mashariki.
0 Maoni