Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema kukamilika kiwanda cha kusarifu Mwani
Chamanangwe kitakuwa na uwezo wa kununua tani
30,000 za Mwani kwa wakulima.
Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipoweka Jiwe la Msingi
Kiwanda cha kusarifu Mwani Chamanangwe Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba
tarehe 05 Januari 2024.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa kiwanda hicho
kitapokamilika ajira zitapatikana, bei itapanda pamoja na soko la uhakika la
nje kutokana na kusarifu hapa nchini.
Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi amesema Serikali itaendelea
kuwawezesha Wakulima wa Mwani kwa kuwapatia maboti , mashine pamoja na zana
mbalimbali za kuzalisha Mwani ili kuongeza
uzalishaji kwa wingi wa Mwani.
Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa kujengwa
kiwanda hicho ambacho ni kikubwa Afrika inatokana pia kuwa Zanzibar ni nchi
inayoongoza kwa kuzalisha zao hilo Afrika.
Vilevile amesema kuwa Mikoa ya Tanzania Bara ya mwambao ikiwemo Mtwara, Tanga wako tayari kuuza Mwani Zanzibar.
0 Maoni