Waziri Nape Aipongeza Huawei Kwa Programu ya “Seed for the Future”

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Moses Nnauye ameipongeza Kamapuni ya Huwawei kwa kuwezesha  programu ya “Seed for the Future” inayochochea Vijana wa Kitanzania kushiriki kikamilifu katika Teknolojia za Kidijitali ambao wamehitimu mafunzo maalumu kuhusu program hiyo.

Mhe. Nape ametoa pongezi hizo wakati akizungumza katika hafla ya kuwakabidhi vyeti vya kukamilisha mafunzo maalumu iliyoshirikisha Vijana 14. Hafla hiyo imefanyika katika Hoteli ya Rotana Jijini Dar es Salaam.

Kampuni ya Huawei ilizindua programu yake ya kimataifa inayowawezesha vijana kushiriki katika mafunzo ya teknolojia ya kidijitali.

Waziri Nape Nnauye aliipongeza Huawei kwa juhudi zao na kuonyesha mipango na matumaini kuhusu athari chanya zinazotokana na programu hiyo kwa vijana wa Tanzania.

Waziri Nape Nnauye alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, makampuni binafsi, na Taasisi za Elimu ya Juu katika kuendeleza ujuzi wa kidijitali miongoni mwa vijana.

Alizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,  Bwana Mohammed Khamis Abdullah pia amewapongeza Huawei kwa kutoa fursa kwa vijana wa Tanzania kwa kuwawezesha katika ubunifu wa kimataifa na kuwezesha nia ya  Serikali ya kukuza ujasiriamali kupitia ubunifu kapitia TEHAMA.

“Seeds for the Future” ni programu muhimu kwa maendeleo ya kidijitali nchini Tanzania. Programu hii inalenga kuwawezesha vijana kushiriki katika ujenzi wa mustakabali wa kidijitali wenye nguvu kuwezesha uchumi wa kidijitali na maendeleo ya nchi kwa ujumla

Chapisha Maoni

0 Maoni