Wakazi wa Kijiji cha Sebasi
Wilayani Hanang Mkoani Manyara wamehimizwa kuendelea kuzingatia kanuni
za afya, ikiwemo kutumia maji yaliyotibiwa na vidonge vya klorine ili kuweza
kuepuka magonjwa ya kuharisha na kutapika.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Sehemu ndogo ya Maji na Usafi
wa Mazingira kutoka Wizara ya Afya Anyitike Mwakitalima baada ya kutembelea
katika kijiji Sebasi Wilayani Hanang Mkoani Manyara ikiwa ni mwendelezo wa
kuhakikisha kanuni za usafi wa mazingira zinazingatiwa katika kujikinga na
Magonjwa ya mlipuko.
“Kwa sehemu kubwa miundombinu ya maji imeathiriwa hivyo wito
tunaotoa haya maji yanayotolewa ni kuyatibu ili yawe safi na salama kwa ajili
ya kujikinga na magonjwa ya mlipuko na jamii imeitikia mwito inatumia maji
yaliyowekewa dawa ya kutibu maji,”amesema Mwakitalima.
Aidha, Mwakitalima amehimiza umuhimu wa utumiaji wa wananchi
kutumia vyoo na kunawa mikono kwa sabuni mara watokapo kujisaidia pamoja na
kunawa mikono wakati wa kula ili kulinda afya zao.
Kwa upande wao wanakijini wa Sebasi wamesema elimu ya afya inayoendelea kutolewa ikiwemo utumiaji wa dawa ya kutibu maji, umuhimu wa kutumia choo,inasaidia wao kujikinga na magonjwa ya mlipuko.
0 Maoni