Rais Samia atoa msamaha kwa wafungwa 2,244

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametoa msamaha kwa wafungwa 2,244 katika kuadhimisha miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania bara hii leo.

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema kati ya wafungwa hao wafungwa 263 wataachiwa huru leo, wafungwa 2 waliohukumiwa adhabu ya kifo wamebadilishiwa adhabu hiyo na kuwa kifungo cha maisha.

Pamoja na mambo mengine taarifa hiyo ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema pia wafungwa 1,979 wamepunguziwa sehemu ya adhabu zao ambazo wataendelea kuzitumikia gerezani.


Chapisha Maoni

0 Maoni