Rais Dk. Mwinyi akutana na Mwenyekiti wa Chama cha Wajane Afrika

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Mwenyekiti wa Chama  cha Wajane Afrika (TAWS), Hope Nwakwesi na ujumbe wake Ikulu Zanzibar tarehe:19 Desemba 2023.

Aidha , Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali inathamini haki za wajane.

Naye, Mwenyekiti wa Wajane Afrika Hope Nwakwesi amemweleza Mh.Rais Dk. Mwinyi kuhusu kufanyika Zanzibar mkutano mkubwa wa Wajane Afrika utakaoshirikisha  nchi zaidi ya 54  kuanzia tarehe 20,21 na 22 Juni mwaka 2024.

Mkutano huo utajadili changamoto, masuala yanayohusu wajane na kutafuta ufumbuzi.

Halikadhalika Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali itajitahidi kusimamia kuhakikisha mkutano huo unakwenda vizuri.

Chapisha Maoni

0 Maoni