Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Mwenyekiti wa Chama cha Wajane Afrika (TAWS), Hope Nwakwesi na
ujumbe wake Ikulu Zanzibar tarehe:19 Desemba 2023.
Aidha , Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali inathamini haki za
wajane.
Naye, Mwenyekiti wa Wajane Afrika Hope Nwakwesi amemweleza
Mh.Rais Dk. Mwinyi kuhusu kufanyika Zanzibar mkutano mkubwa wa Wajane Afrika
utakaoshirikisha nchi zaidi ya 54 kuanzia tarehe 20,21 na 22 Juni mwaka 2024.
Mkutano huo utajadili changamoto, masuala yanayohusu wajane
na kutafuta ufumbuzi.
Halikadhalika Rais Dk. Mwinyi amesema Serikali itajitahidi kusimamia kuhakikisha mkutano huo unakwenda vizuri.
0 Maoni