Waziri wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima na Jumuiya
ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wamejadili kuimarisha ushirikiano kwenye
ajenda za kuendelea kumkomboa Mwanamke Kiuchumi, kiongozi, kijamii na kupambana
na ukatili wa kijinsia.
Akizungumza na Katibu Mkuu
wa UWT Ndugu Jokate Mwegelo Ofisi za Makao Makuu Jijini Dodoma 21 Novemba, 2023
Dkt. Gwajima amesema wameweza kujadiliana juu ya mipango mbalimbali ya kisekta
inayohusu kumkomboa mwanamke katika nyanja mbalimbali ikiwa ni dhamira ya dhati
ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na Chama Cha
Mapinduzi.
Aidha, masuala mengine
yaliyojadiliwa ni pamoja na kuendelea kuhakikisha Wanawake wanainuliwa kiuchumi
ikiwa ni dhamira thabiti ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan katika kujenga na kuimarisha jamii iliyo bora na rafiki kwa
Watoto na Wanawake wote nchini.
0 Maoni