Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha katika ajali ya Basi
la Kampuni ya Ally's lenye namba za usajili T 178 DVB lililoigonga treni ya
mizigo Manyoni Mkoani Singida.
Taarifa zilizotufikia zinasema basi hilo lililokuwa
likitokea Dar es Salaam kwenda Mwanza liliigonga treni ya mizigo katika eneo la
Manyoni leo Novemba 29, 2023 majira ya Saa 11 alfajiri.
0 Maoni