Muhimbili kuendelea kuwa kinara utoaji huduma bora za afya nchini

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Prof. Mohamed Janabi amesema hospitali hiyo itaendelea kuimarisha huduma bora kwa mteja ili kuwavutia watu wengi ndani na nje ya nchi kuja kutibiwa Muhimbili.

Prof. Janabi amaeyasema hayo alipokua akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel alipotembelea Muhimbili a kufanya kikao na wakuu wa Taasisi za afya ikiwemo MNH, JKCI, MOI, MSD, NHIF, TMDA, Mganga Mkuu wa Mkoa pamoja na Waganga Wafawidhi wa Hospitali za Rufaa za mkoa wa Dar es Saalam.

Prof. Janabi amesema tofauti kubwa iliyopo katika Hospitali za Umma kwa sasa ni suala la huduma bora kwa mteja kwani serikali imewezesha kuwepo kwa vifaa tiba vya kisasa vyenye ubora hali ya juu na wataalamu hivyo hatuna budi kuzingatia suala la kutoa huduma bora kwa mteja.

Akielezea mafanikio ya Muhimbili amesema chini ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita MNH, imeendelea kutoa huduma za kibingwa na kibobezi ambapo hivi karibuni kwa upande wa Muhimbili Mloganzila jumla ya wagonjwa 7 wamepandikizwa figo na mwishoni mwa mwezi huu itaweka kambi maalumu ya kupandikiza nyonga na magoti kwa wagonjwa wenye changamoto hizo.

Aidha, Prof. Janabi ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi kujiunga na bima ya afya kabla hawajaumwa kwakua matibabu ni gharama na kusisitiza kuwa huduma za afya zinapaswa kuchangiwa ili kuwa endelevu.

Chapisha Maoni

0 Maoni