Wataalamu kutoka Taasisi ya
Weill Cornel ya nchini Marekani wametembelea Hospitali ya Taifa
Muhimbili-Mloganzila kwa lengo la kujionea miundombinu ya kutolea huduma na
kukutana na wataalamu ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa taasisi hiyo
kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili (Upanga & Mloganzila)
kuimarisha kitengo cha kutibu kiharusi (Stroke Unit).
Awali wataalamu hao
walikutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed
Janabi ambaye alisema kuwa mpango huo utakuwa na manufaa makubwa kwa kuwa utasaidia
matibabu kwa watu waliopata kiharusi ndani ya saa 24 za mwanzo.
Alisema kuwa Muhimbili
inavifaa tiba vya kisasa vya kuhudumia wagonjwa wa kiharusi ikiwemo mtambo wa
Angio-Suite ambao hutumika kufanya uchunguzi na matibabu ya kiharusi, pamoja na
wataalamu wabobezi wa kutibu kiharusi.
0 Maoni