Watu wapatao 16 wanahofiwa kufa katika tukio la kushambuliwa
kwa risasi kwenye mji wa Lewiston, Maine nchini Marekani.
Polisi wa mji huo wamemtaja mtuhumiwa wa mashambulizi hayo
kuwa ni Robert Card mwenye umri wa miaka 40, na kusema kuwa anasilaha na ni mtu
hatari.
Mji huo mdogo wa Lewiston, Maine umefungwa, wafanyabiashara
wameambiwa wafunge biashara zao na watu wameagizwa kukaa nyumbani.
Mamia ya maafisa wa polisi wapo katika msako mkali wa
kumtafuta mtuhumiwa huyo aliyefanya mauaji hayo kwenye hoteli na eneo la
michezo wa shabaha ya kulenga chupa.
0 Maoni