Watu waliokufa kwa shambulizi lililofanya na kundi la Hamas
nchini Israel wamefikia 1,200, huku pia watu 900 wakiuawa huko Gaza katika
mashambulizi ya Israel ya kulipa kisasi.
Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Israel amesema picha
zinazotoka Gaza zitakuwa ni vigumu kwa mtu kushuhudia.
Wakati huo huo ndege ya kwanza ya Marekani iliyobeba silaha
imewasili kusini mwa Israel kupeleka msaada wa silaha.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amempigia simu Rais
wa Marekani Joe Biden na kumshukuru kwa kuiunga mkono Israel.
0 Maoni