DC Kwimba aitaka RUWASA kutatua changamoto ya maji

 

Mkuu wa wilaya ya Kwimba Ngw'ilabuzu Ludigija ameiagiza wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA kutatua changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama kwa wakazi wa kata za Shilembo na Ilula kwa kuvuta maji kutoka maeneo jirani au kuchimba visima ili wakazi hao wapate maji.

Akiwa katika mwendelezo wa kusikiliza na kutatua kero za wakazi hao Ludigija amesema maji ni muhimu hivyo RUWASA wanatakiwa kufanya jitihada za kuhakikisha maji yanafika kwa wakazi wa kata hizo.

"Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan anaendelea kuleta fedha za miradi ya maji ili kumtua mama ndoo kichwani sasa niwatake RUWASA muangalie uwezekano wa kufikisha maji hapa," amesema Ludigija.

Akizungumza mwa niaba ya wakazi wa kata hizo Mwalu Joseph amesema wamekuwa wakitumia muda mwingi kutafuta maji na kushindwa kufanya shughuli zingine za maendelo.

"Tunateseka sana kupata maji tunatembea zaidi ya kilometa tisa kwenda kutafuta maji tunamuomba Rais atusaidie tupate japo visima au amji ya Ziwa Victoria ili tuepukane na adha hii," amesema Mwalu.


Mmoja wa wakinamama ambaye ni mkazi wa kata ya Shilembo akiwa na baiskeli yake kwenda kutafuta maji ambayo yamekuwa ni kero kubwa katika kata hiyo pamoja na ya Ilula wilayani Kwimba.



Chapisha Maoni

0 Maoni