Hali ya taharuki imeibuka baada ya Chama cha Wanasheria
Kenya kubaini kuwa mwanaume mmoja anayefanya shughuli ya uwakili si wakili na
wala hana leseni ya kuwa wakili wa Mahakama Kuu.
Wakili huyo kanjanja Brian Mwenda Njagi amesimamia kesi 26
katika Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Rufaa na kushinda
kesi zote hizo.
Njagi anayedai kuwa ni wakili wa Nairobi, alikamatwa jana na
mamlaka za nchi hiyo kwa kujifanya kuwa wakili wa Mahakama Kuu ya Kenya.
Kikosi maalum Chama cha Wanasheria Kenya tawi la Nairobi RAT,
kilimkamata Njagi baada ya kupata malalamiko ya watu kuwa ni laghai.
Baada ya kusamba taarifa za kukamatwa kwake, baadhi ya Wakenya
kupitia mitandao ya jamii wamekuwa wakimpongeza wakili huyo kwa kuwa na uwezo
mkubwa wa kisheria kuliko waliosomea.
0 Maoni