Wanamgambo wa Kiislamu wameshambulia boti kwenye mto
kaskazini mashariki mwa Mali, na kuua raia wapatao 49, Serikali ya mpito ya
nchi hiyo imesema.
Pia, imeripotiwa kikundi hicho kimeshambulia kambi ya jeshi,
na kuwaua wanajeshi 15, huku pia wapiganaji hao wapatao 50 wakiuawa.
Kufuatia mauaji hayo Serikali ya mpito ya Mali, imetangaza
siku tatu za maombolezo.
0 Maoni