Waliojenga mabondeni watahadharishwa ujio wa mvua za El Nino

 

Serikali imewatahadharisha wananchi kuacha kujenga na kufanya shughuli za kijamii kwenye maeneo ya mabondeni, ili kuepukana na athari za mafuriko zinazoweza kutokea na kusababisha madhara, pindi zinyeshapo mvua kubwa kama za El Nino.

Tahadhari hiyo imetolewa bungeni leo na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati akijibu maswali bungeni Jijini Dodoma leo Septemba 05,2023.

" Nikweli panapokuwa na mvua kubwa kama za El Nino mara nyingi hutokea madhara ambayo yanaharibu makazi na kugharimu maisha ya watu, hivyo Serikali katika kipindi hiki tunawapa elimu wasijenge kwenye maeneo ambayo yanakaa maji na kama wanampango huo basi waondoke ili mvua zitakaponyesha wasipate madhara," alisema Mhe. Khamis.

Hivi karibuni Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilitangaza kuanza kwa mvua za El Nino Oktoba hadi Desemba 2023 na kutahadharisha kuweza kusababisha madhara kwa binadamu na mazingira ikiwemo mafuriko.

Chapisha Maoni

0 Maoni