Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ameonyesha
kutofurahishwa na vinara wa biashara za magendo ambao hupitisha bidhaa
mbalimbali katika Bandari bubu pasipo kulipa kodi ambapo amesema hali hiyo
haivumiliki hawezi kuifumbia macho hata kidogo.
RC Chalamila amebainisha hayo baada kutembelea na kukagua
kipenyo mama cha Magendo eneo la Kunduchi na Bandari ndogo ya Mbweni Wilaya ya
Kinondoni.
Chalamila amesema kuendelea kuacha mianya hiyo ya magendo ni
kuikosesha kodi Serikali, kuhatarisha Afya za wananchi kutokana na kutumia
bidhaa ambazo hazija thibitishwa usalama wake na mamlaka husika ikiwemo TBS
vilevile ni hatari kwa usalama wa Taifa "Hivi karibuni wako watu walipata
itilafu ya kiafya kutokana na matumizi ya mafuta ya magendo siwezi vumilia hali
hiyo".
Vilevile RC Chalamila ametoa siku mbili kwa wachuuzi wa eneo
la fukwe ya kunduchi kujitafakari kwa sababu haiwezekani bidhaa hizo zinapita
hapo alafu wasijue ambapo amewataka kufanya biashara halali Mhe Rais Dkt Samia
Suluhu amewekeza nguvu kubwa kutengeneza nchi hivyo wananchi ni lazima
waungunge mkono juhudi hizo kwa kukataa magendo kwa masilahi mapana ya Mkoa na
Taifa.
Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule amekiri
kuwepo kwa Changamoto hiyo na amekuwa akipambana kwa kushirikiana na Mamlaka
huisika TRA TBS, na Bandari pamoja na vyombo vya dora lakini namna pekee ni
kuendelea na kuongeza nguvu katika ulinzi na kufanya Doria katika mianya hiyo
hakuna kinachoshindikana inawezekana kinachotakiwa ni kutimiza wajibu wa kila
mmoja wetu.
0 Maoni