Majengo marefu yanaungua moto katika Jiji la Sudan, baada ya
mapigano makali baina ya vikosi vya majeshi vinavyokinzani nchini humo.
Video iliyopostiwa kwenye mitandao inaonyesha jengo refu la
kampuni ya mafuta ya Greater Nile Petroleum Oil likiwa linawaka moto.
Mashambulizi ya anga na yaaridhini yamekuwa yakiendelea
Jijini Khartoum pamoja na kwenye miji mingine tangu mapigano hayo yaanze mwezi Aprili,
2023.
Mapigano hayo ya baina ya vikosi viwili vya jeshi la nchi
hiyo vilivyohitilafiana yamepelekea watu zaidi ya milioni moja kukimbia nchi
hiyo.
0 Maoni