Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi akiambatana na Mama Mariam Mwinyi pamoja na ujumbe wake
amewasili leo Havana, Cuba kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa
kundi la 77 na China (G77+China)
Mkutano huo unatarajiwa kufunguliwa kesho tarehe 15 Septemba
ambapo Rais Dk. Mwinyi atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Katika uwanja wa ndege wa Jose Marti Rais Dk. Mwinyi
alipokelewa na Balozi wa Tanzania Mhe.
Humphrey Polepole na maafisa wengine wa ubalozi wa Tanzania Havana,
Cuba.
Baadae leo Rais Dk. Mwinyi atafungua rasmi ubalozi wa
Tanzania nchini Cuba.
0 Maoni