Chama cha Tanzania Bloggers Network (TBN) leo kimekutana na
Afisa wa masuala ya Umma Bi Jeanne Clark pamoja na Bi. Kalisha Holmes, Afisa
Habari na Mawasiliano wa Ubalozi wa Marekani katika kikao kisicho rasmi
kilichoambatana na chakula cha mchana katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, wanachama waandamizi wa TBN
waliohudhuria walieleza mipango inayoendelea ya kukiendeleza chama chao ili
kukuza kazi nzuri inayotekelezwa na chama hicho kilichozinduliwa mwanzoni mwa
mwaka 2015.
Maafisa hao wa ubalozi wamesema wanavutiwa na kazi
zinazofanywa na wanahabari mitandaoni na wameelezea nia ya kishirikiana na TBN
katika mafunzo ili kukuza taaluma kwa kuzingatia weledi na miiko ya uanahabari.
0 Maoni