Kiungo wa Kimataifa wa Tanzania, Novatus Dismas Miroshi, anaenda
kuwa mchezaji wa pili kutoka Tanzania kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa
Ulaya (UEFA), baada ya Mbwana Samatta.
Novatus mwenye umri wa miaka 21 amepata nafasi hiyo baada ya
kujiunga na klabu ya Shakhtar Donesk ya Ukraine akitokea klabu ya Zulte Waregem
ya Ubelgiji.
Kwa hiyo kiungo huyo wa Stars, atacheza UEFA Champions
League akiwa na timu yake mpya ambayo ipo kundi H pamoja na timu za Barcelona,
Porto na Royal Antwer.
0 Maoni