Watu wapatao 100 wamekufa na wengine 150 wamejeruhiwa, baada
ya moto kutokea kwenye harusi kaskazini mwa nchi ya Irak, chombo cha habari cha
umma kimeripoti.
Haijafahamika mara moja chanzo cha moto huo, lakini taarifa
za awali zinasema moto huo umetokea baada ya kufyatuliwa fataki.
Picha katika mitandao ya jamii zinaonyesha mabaki ya ukumbi
uliofanyika harusi hiyo kwenye mji wa Al-Hamdaniya
katika mkoa wa Nineveh.
Vifaa vilivyotumika kujengea ukumbi huo vyenye uwezo wa
kuwaka moto vimeelezwa kwamba vilichangia kuuchochea moto huo, maafisa wa Irak
wamesema.
Haijajulikana bado iwapo maharusi na wapambe wao kuwa ni
miongoni mwa watu waliokufa ama kujeruhiwa katika tukio hilo la ajali ya moto.
0 Maoni