Kiongozi wa kundi la mrengo mkali wa kulia la Proud Boys
amehukumiwa kifungo cha miaka 17 jela, kikiwa ni moja ya kifungo cha muda mrefu
kwa kuhusika na uvamizi katika jengo la US Capitol 2021.
Mwanajeshi huyo veteran wa Marekani Joe Biggs, 38, alihusika
katika kuchochea tukio la kuvamia kikoa cha Baraza la Congress wJanuaria 6, 2021.
Biggs ambaye aliwahi kuwa mwandishi wa kujitegemea wa tovuti
ya habari feki ya Infowars ametiwa hatiani kwa makossa ya uchochezi na kula
njama, pamoja na mashtaka mengine mwezi Mei.
Mwanachama mwingine wa kundi la Proud Boys, Zachary Rehl, alihukumia
kwenda jela miaka 15, siku ya Alhamisi kwa makosa ya uchochezi na kula njama.
Januari 6, 2021 kundi la Proud Boys liliongoza tukio la
kuvamiwa kwa jengo la Capitol katika jitihada za kushinikiza Baraza la Congress
lisiidhinishe ushindi wa Rais Joe Biden.
0 Maoni