Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, amesema moto ulioleta maafa katika Jiji la Johannesburg umetoa funzo kwa taifa hilo.
Watu 74 wamekufa wakiwamo watoto 12, baada ya moto huo
kuunguza jengo la ghorofa walimokuwa wanaishi watu wasionamakazi, wengi wao
wakiwa wahamiaji.
Watu wengine zaidi ya 50 wamejeruhiwa katika tukio hilo la
ajali ya moto mbaya iliyozishtua mamlaka za Jiji.
Mapema jana, mamlaka ya Jiji la Johannesburg ilithibitisha
kumiliki jengo hilo, ambalo imesema lilikuwa limetwaliwa na genge.
0 Maoni