Newcastle United imepangwa kuvaana na miamba ya Ulaya Paris
St-Germain, Borussia Dortmund na AC Milan katika kundi F la Ligi ya Mabingwa
Ulaya (UEFA).
Newcaste iliyotinga katika michuano hiyo kwa mara ya kwanza
tangu 2002-2003, inakutana na vigogo hao wa soka ambao wote wamewahi kufika
fainali za michuano hiyo katika miaka 16 iliyopita.
Manchester United yenyewe imepangiwa kuivaa Bayern Munich, huku
mabingwa watetezi wa michuano hiyo Manchester City wapo kwenye kundi moja na RB
Leipzig.
Kwa upande wao timu ya Arsenal wamepangiwa kukutana na Sevilla
huko nao Celtic wakikkutana na Atletico Madrid.
0 Maoni