Rais wa Shirikisho la Soko la Hispania Luis Rubiales
amejiuzulu wadhifa wake kufuatia kukosolewa kwa kumbusu mchezaji Jenni Hermoso
wakati wa sherehe za ushindi wa Kombe la Dunia la Wanawake.
Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Hispania Hermoso, 33, amesema
busu hilo alilopigwa baada ya Hispania kuifunga England, halikuwa la hiyari na
ameshafungua mashtaka jumanne ya wiki iliyopita.
Katika taarifa yake Rubiales amesema amewasilisha barua yake
ya kujiuzulu urais Shirikisho la Soko la Hispania kwa kaimu rais wa shirikisho
hilo Pedro Rocha.
0 Maoni