Bosi wa kundi la Mafia, Matteo Messina Denaro, ambaye
alikuwa ni mhalifu anayetafutwa mno hadi alipotiwa nguvuni mwaka huu, afariki.
Denaro mwenye miaka 61, inaaminika kuwa ni bosi wa kundi
hatari la Cosa Nostra Mafia alikuwa akivikimbia vyombo vya dola kwa miaka 30,
hadi aliponaswa Januari mwaka huu.
Matteo Messina Denaro, alikuwa akitibiwa saratani wakati
akiwa kizuizini na alihamishwa kutoka gerezani na kupelekwa hospitali mwezi
huu.
Denaro anahusishwa na mauaji ya watu wengi, na aliwahi kunukuliwa
akisema kwamba atayajaza makaburi miili ya maadui zake.
0 Maoni