Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imejizatiti kutimiza ahadi na malengo ya
Ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2020-2025 ya kuzalisha fursa mbalimbali za ajira
ikiwemo uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na wajibu wa Serikali kuandaa mazingira
wezeshi ili kuinua fursa hizo.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 25 Septemba 2025
wakati akifungua Tamasha la kwanza la Fahari ya Zanzibar na mwaka mmoja wa
Taasisi ya Wakala wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) katika
ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa Serikali imeendelea na
hatua za kuimarisha miundombinu ya mazingira ya kufanyia biashara kwa
wajasiriamali ikiwemo ujenzi wa masoko na vituo vya mabasi.
Vilevile, amesema uchumi wa Zanzibar una fursa nyingi za
masoko kwa kuwepo kwa hoteli nyingi za kitalii kwa mahitaji ya bidhaa
mbalimbali hivyo amewataka wadau wanaojihusisha na sekta ya utalii kuhakikisha
wajasiriamali wazawa wananufaika na fursa hizo.
Halidhalika Rais Dk. Mwinyi ametoa wito kwa wajasiriamali
hao kuzalisha bidhaa kwa viwango vinavyohitajika ili kupunguza uingizaji wa
bidhaa za nje ili kuimarisha soko la ndani.
0 Maoni