Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb),
amesema Wizara inaandaa utaratibu mzuri kwa ajili ya kuongoza shughuli za
uwindaji wa kienyeji.
Waziri Mchengerwa ameyasema hayo, jana alipotembelea banda
la TAWA katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu
Julius Nyerere (Nanenane), Mkoani Morogoro.
Waziri Mchengerwa amesema utaratibu huo utawekwa kwa ajili ya
watanzania wanaopenda kufanya shughuli za uwindaji na utaendelea kusimamiwa na
TAWA.
Sambamba na hilo, Waziri Mchengerwa amesisitiza kuendelea
kutangaza vivutio vya utalii pamoja na kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha
mchango wa utalii katika pato la Taifa unaongezeka.
"Mchango wetu katika pato la Taifa unakaribia shilingi
Trillion Saba, tunataka tutoke Trillion Saba hadi Trillioni kumi, tukifanya
kazi kwa bidii inawezekana" amesema Waziri Mchengerwa.
TAWA inashiriki katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea
katika Mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kutangaza shughuli zake sambamba na
fursa mbalimbali za uwekezaji ikiwemo ufugaji wa wanyamapori.
0 Maoni